Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa: Si sera ya Serikali kuwaonea waandishi wa habari
Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Si sera ya Serikali kuwaonea waandishi wa habari

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema, sio sera ya Serikali kuwaonea waandishi wa habari wanaotekeleza majukumu yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro…(endelea).

Majaliwa amesema hayo leo Alhamisi, tarehe 20 Mei 2021, katika mkutano wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), uliofanyika mkoani Morogoro.

Ametoa kauli hiyo, baada ya jukwaa hilo kuwasilisha kwake malalamiko ya baadhi ya waandishi wa habari, kushambuliwa na maafisa wa Serikali wakitekeleza majukumu yao.

Majaliwa amesema, Serikali haitavumilia mtu yeyote atakayemkwaza mwandishi wa habari wakati wa utekelezaji majukumu yake.

“Wala sio sera ya serikali kuonena waandishi wa habari, serikali haitavumilia mtu yeyote atakayemkwaza mwandishi wa habari akiwa katika kazi ya uandishi wa habari na niwahakikishie kuwa, hatua kali itachukuliwa dhidi yake,” amesema Majaliwa.

Waziri mkuu huyo amesema, Serikali itaendelea kulinda misingi ya habari huku akiwataka wadau wa tasnia hiyo kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.

“Serikali itaendelea kuimarisha misingi ya habari tuliyo nayo nchini, kwa upande wenu zingatieni sheria za nchi, msitumie vibaya kalamu zenu. Ni muhimu sana kalamu yenu itumike kusimamia haki ya kila mmoja,” amesema Waziri Majaliwa.

Tarehe 21 Aprili 2021, Mwandishi wa Habari wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), Jesse Mikofu, alishambuliwa na baadhi ya askari wa Vikosi vya Jeshi la Polisi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), akitekeleza majukumu yake.

Mwandishi huyo alikumbwa na mkasa huo, baada ya kuwapiga picha askari hao waliokuwa wanatekeleza jukumu la kuwahamisha wamachinga waliopanga bidhaa zao barabarani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!