Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa: Si sera ya Serikali kuwaonea waandishi wa habari
Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Si sera ya Serikali kuwaonea waandishi wa habari

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema, sio sera ya Serikali kuwaonea waandishi wa habari wanaotekeleza majukumu yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro…(endelea).

Majaliwa amesema hayo leo Alhamisi, tarehe 20 Mei 2021, katika mkutano wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), uliofanyika mkoani Morogoro.

Ametoa kauli hiyo, baada ya jukwaa hilo kuwasilisha kwake malalamiko ya baadhi ya waandishi wa habari, kushambuliwa na maafisa wa Serikali wakitekeleza majukumu yao.

Majaliwa amesema, Serikali haitavumilia mtu yeyote atakayemkwaza mwandishi wa habari wakati wa utekelezaji majukumu yake.

“Wala sio sera ya serikali kuonena waandishi wa habari, serikali haitavumilia mtu yeyote atakayemkwaza mwandishi wa habari akiwa katika kazi ya uandishi wa habari na niwahakikishie kuwa, hatua kali itachukuliwa dhidi yake,” amesema Majaliwa.

Waziri mkuu huyo amesema, Serikali itaendelea kulinda misingi ya habari huku akiwataka wadau wa tasnia hiyo kutekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.

“Serikali itaendelea kuimarisha misingi ya habari tuliyo nayo nchini, kwa upande wenu zingatieni sheria za nchi, msitumie vibaya kalamu zenu. Ni muhimu sana kalamu yenu itumike kusimamia haki ya kila mmoja,” amesema Waziri Majaliwa.

Tarehe 21 Aprili 2021, Mwandishi wa Habari wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), Jesse Mikofu, alishambuliwa na baadhi ya askari wa Vikosi vya Jeshi la Polisi vya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), akitekeleza majukumu yake.

Mwandishi huyo alikumbwa na mkasa huo, baada ya kuwapiga picha askari hao waliokuwa wanatekeleza jukumu la kuwahamisha wamachinga waliopanga bidhaa zao barabarani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!