Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanesco yaomba radhi, yaeleza huduma za luku zinapopatikana
Habari Mchanganyiko

Tanesco yaomba radhi, yaeleza huduma za luku zinapopatikana

Spread the love

 

SHIRIKA la Umeme Tanzania (Tanesco), limewaomba radhi wateja wake kutokana na ukosefu wa huduma ya ununuzi wa luku kwa njia ya mtandao na kusema, huduma hiyo, inapatikana ofisi zake za mikoa na wilaya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Huduma hiyo, imekuwa adimu kwa siku ya tatu na leo Jumatano, tarehe 19 Mei 2021, Tanesco imetoa taarifa ikisema, huduma hiyo kwa sasa inatikana ofisi za mikoa na wilaya.

Limesema, wataalamu wa shirika hilo, wanaendelea na kazi ya utatuzi wa manunuzi kupitia njia za kielektroniki.

“Tunaomba uvumilivu wakati wataalamu wetu wakiendelea na kazi kuhakikisha tatizo hilo linatatuliwa,” imeeleza taarifa hiyo ya Tanesco huku ikiongeza “tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!