Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi asamehe wafungwa 49
Habari za Siasa

Rais Mwinyi asamehe wafungwa 49

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Hussein Mwinyi, ametoa msamaha kwa wafungwa 49, waliokuwa wakitumikia magereza ya Unguja na Pemba. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Msamaha huo unakwenda sambamba na shamra shamra za sherehe za miaka 57 ya Mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika leo Jumanne tarehe 12 Januari 2021.

Rais Mwinyi ametoa msamaha huo kwa mujibu wa kifungu cha 59 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kinachompa mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa waliofungwa gerezani.

Kutokana na msamaha huo, Rais Mwinyi ameamuru kifungo kilichobaki cha wafungwa hao walionufaika na msamaha kuwa kipindi hicho chote kinafutwa na waachiwe huru kuanzia jana Jumatatu tarehe 11 Januari 2021.

Kati ya wafungwa hao 49; 46 walikuwa magereza ya Unguja na watatu Pemba.

Msamaha huo hutolewa kila mwaka katika kipindi cha sherehe za Mapinduzi matukufu, huwahusisha wafungwa ambao ni wazee sana, wenye maradhi sugu au wenye makosa madogo ambao wamebakisha muda mfupi wa kutumikia adhabu zao, wanaoonesha nidhamu nzuri chuoni na kujutia makosa yao.

Wafungwa wenye makosa kama vile kuua kwa makusudi, wizi wa kutumia nguvu, wizi wa mali ya umma, makosa ya kudhalilisha wanawake na watoto, makosa ya dawa za kulevya na wenye makosa mengi ya zamani kwa kawaida huwa hawapewi msamaha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za Siasa

Askofu Shoo awataka ACT kupigania maslahi ya Taifa, wasikubali kuhongwa

Spread the loveALIYEKUWA Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri, Askofu...

Habari za Siasa

Biteko aagiza waajiri kudhibiti vifo mahali pa kazi

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!