Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi asamehe wafungwa 49
Habari za Siasa

Rais Mwinyi asamehe wafungwa 49

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Hussein Mwinyi, ametoa msamaha kwa wafungwa 49, waliokuwa wakitumikia magereza ya Unguja na Pemba. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Msamaha huo unakwenda sambamba na shamra shamra za sherehe za miaka 57 ya Mapinduzi ya Zanzibar zilizofanyika leo Jumanne tarehe 12 Januari 2021.

Rais Mwinyi ametoa msamaha huo kwa mujibu wa kifungu cha 59 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kinachompa mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa waliofungwa gerezani.

Kutokana na msamaha huo, Rais Mwinyi ameamuru kifungo kilichobaki cha wafungwa hao walionufaika na msamaha kuwa kipindi hicho chote kinafutwa na waachiwe huru kuanzia jana Jumatatu tarehe 11 Januari 2021.

Kati ya wafungwa hao 49; 46 walikuwa magereza ya Unguja na watatu Pemba.

Msamaha huo hutolewa kila mwaka katika kipindi cha sherehe za Mapinduzi matukufu, huwahusisha wafungwa ambao ni wazee sana, wenye maradhi sugu au wenye makosa madogo ambao wamebakisha muda mfupi wa kutumikia adhabu zao, wanaoonesha nidhamu nzuri chuoni na kujutia makosa yao.

Wafungwa wenye makosa kama vile kuua kwa makusudi, wizi wa kutumia nguvu, wizi wa mali ya umma, makosa ya kudhalilisha wanawake na watoto, makosa ya dawa za kulevya na wenye makosa mengi ya zamani kwa kawaida huwa hawapewi msamaha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!