Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli ateua wabunge 2
Habari za Siasa

Magufuli ateua wabunge 2

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS Tanzania, John Pombe Magufuli leo tarehe 29 Novemba, 2020 amefanya uteuzi wa wabunge wawili wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kwanza, Rais Magufuli amemteua Humphrey Polepole kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Polepole ni Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Pili, Rais Magufuli amemteua Riziki Said Lulida kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM

Katika Bunge la 11 lililomalizika, Riziki alikuwa mbunge wa viti Maalum kupitia Chama Cha Wananchi (CUF) ambaye mwishoni mwa Bunge hilo, alitangaza kutimkia Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikuku imesema, wabunge wateule hao wataapishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1 Comment

  • Asante ndugu jpm kwa uteuzi wa pole pole fikra zako na uteuzi uo zimeunga na wana ccm na taifa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!