Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aanza kuteua, amteua AG
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli aanza kuteua, amteua AG

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli ameanza kuunda Serikali atakayoiongoza kwa miaka mitano ijayo 2020-2025 kwa kumteua Profesa Adelardus Kilangi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG). Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Uteuzi huo umefanyika leo Alhamisi tarehe 5 Novemba 2020 saa chache kupita tangu Dk. Magufuli alipoapishwa na Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma kuwa Rais wa Tanzania.

Dk. Magufuli na makamu wake, wameapishwa kwa pamoja Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

“Profesa Kilangi ameteuliwa kushika wadhifa huo kwa kipindi cha pili baada ya uteuzi wa kipindi cha kwanza kumalizika leo tarehe 05 Novemba, 2020,” imeeleza taarifa ya Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Profesa Adelardus Kilangi

Kabla ya uteuzi huo, Profesa Kilangi alikuwa AG, wadhifa alioteuliwa tarehe 1 Februari 2018 na Rais Magufuli ili kuchukua nafasi ya George Masaju ambaye alimteua kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Itakumbukwa, mara baada ya Rais Magufuli kuingia Ikulu kwa mara ya kwanza tarehe 5 Novemba 2015, alimteua Masaju kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Masaju alishika wadhifa huo wa AG kuanzia tarehe 3 Januari 2015 alipoteuliwa na Rais wa wakati huo, Jakaya Mrisho Kikwete ili kuchukua nafasi ya Fredrick Werema.

Baada ya Rais Magufuli kuingia madarakani, aliendelea na Masaju kwa kumteua kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) nafasi aliyohudumu hadi tarehe 1 Februari 2018 alipomteua Profesa Kilangi.

Kabla ya uteuzi huo wa Profesa Kilangi kuwa AG, alikuwa Mkurugenzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (St. Augustine University) kituo cha Arusha na pia Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Shughuli za Mkondo wa Juu wa Mafuta (Tanzania Petroleum Upstream Regulatory Authority – PURA).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!