Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga kujipima ubavu kwa Mlandege
Michezo

Yanga kujipima ubavu kwa Mlandege

Spread the love

TIMU Yanga kesho itacheza mchezo wa kujipima nguvu dhidi mabingwa wa Ligi Kuu visiwani Zanzibar, Mlandege katika kujiweka sawa kuwakabili Kagera Sugar kwenye mchezo ujao. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Yanga itacheza mchezo huo majira ya Saa 1 jioni kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamanzi kabla ya kusafiri kwenda mkoani Kagera kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar utakaopigwa siku ya Jumamosi 18 septemba, 2020 kwenye dimba la Kaitaba.

Mchezo huo ambao utakuwa na umuhimu mkubwa kwa Yanga ili kujiweka sawa kwa kuwa imefanya mabadiliko makubwa kwenye kikosi chake ambacho kina wachezaji wapya zaidi ya 12.

Yanga inaingia kwenye mchezo huo, huku ikiwa imeshacheza michezo miwili kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara na kuambulia alama 4, baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City na kutoka sare na Tanzania Prisons.

Mlandege FC wao watatumia mchezo huo kujiweka sawa kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi na michuano ya kimataifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

error: Content is protected !!