Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo ZFF yamlilia ‘Mr White’
Michezo

ZFF yamlilia ‘Mr White’

Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) kupitia rais wake Seif Kombo Pandu imetoa pole na kutuma salamu za rambi rambi kufuatia kifo cha Salim Abdullah Turky ‘Mr White’ ambaye alikuwa mbunge aliyemaliza muda wake katika jimbo la Mpendae, Unguja kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Unguja … (endelea).

Mr White alikutwa na umauti usiku wa kuamkia leo, Terehe 15 Septemba, mjini Unguja.

Katika salamu zake za rambi rambi Rais wa ZFF, Seif Pandu ameeleza kuwa marehemu Turky atakumbukwa katika jitihada za kusaidia mchezo wa mpira wa miguu na baadhi ya timu pale msaada wake utakapohitajika. 

Salim Turky, aliyezaliwa 11 Februari 1963, mjini Unguja, anatarajiwa kuzikwa jioni ya leo, kijijini kwake, Fumba, takribani umbali wa kilomita 65 kutoka jimboni kwake, Mpendae, wilaya ya Mjini Magharibi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!