Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa 16 kuchuana ubunge Arusha Mjini
Habari za Siasa

16 kuchuana ubunge Arusha Mjini

Spread the love

WAGOMBEA 16 wa vyama vya siasa nchini Tanzania, watachukuana kuwania Ubunge wa Arusha Mjini katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Wagombea hao, wameteuliwa leo Jumanne tarehe 25 Agosti 2020 na Msimamizi wa uchaguzi jimbo hilo Arusha Mjini, Dk John Pima.

Walioteuliwa ni mbunge anayetetea nafasi hiyo, Godbless Lema wa Chadema na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo anayegombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Leman na Gambo wanatarajia kuchuana kuwania uwakilishi wa wananchi hao wa Arusha Mjini.

Wagombe wengine ni; Zuberi Mwinyi (ADA- TADEA), Shayo John (ACT- Wazalendo), Husna Kundi(AAFP), Matayo Richard (CCK), Magdalena Shanghai (CUF), Elisante Mjema (Demokrasia Makini), Elizabeth Godfrey (DP), Epsiba Kiwhelu (NCCR- Mageuzi), Mkama Rashid(NRA), Simion Bayo(SAU), Alfred Mollel (UDP) na Elias Sumari(UPDP).

Kampeni za uchaguzi huo zinaanza kesho Jumatano tarehe 26 Agosti 2020 na zitahitimishwa 27 Oktoba 2020 na siku inayofuati itakuwa ni Uchaguzi Mkuu.

1 Comment

  • Nimefurahi kuona wamepiga picha ya pamoja ,lakini wasimamizi was uchaguzi watende haki

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!