Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa 16 kuchuana ubunge Arusha Mjini
Habari za Siasa

16 kuchuana ubunge Arusha Mjini

Spread the love

WAGOMBEA 16 wa vyama vya siasa nchini Tanzania, watachukuana kuwania Ubunge wa Arusha Mjini katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Wagombea hao, wameteuliwa leo Jumanne tarehe 25 Agosti 2020 na Msimamizi wa uchaguzi jimbo hilo Arusha Mjini, Dk John Pima.

Walioteuliwa ni mbunge anayetetea nafasi hiyo, Godbless Lema wa Chadema na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo anayegombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Leman na Gambo wanatarajia kuchuana kuwania uwakilishi wa wananchi hao wa Arusha Mjini.

Wagombe wengine ni; Zuberi Mwinyi (ADA- TADEA), Shayo John (ACT- Wazalendo), Husna Kundi(AAFP), Matayo Richard (CCK), Magdalena Shanghai (CUF), Elisante Mjema (Demokrasia Makini), Elizabeth Godfrey (DP), Epsiba Kiwhelu (NCCR- Mageuzi), Mkama Rashid(NRA), Simion Bayo(SAU), Alfred Mollel (UDP) na Elias Sumari(UPDP).

Kampeni za uchaguzi huo zinaanza kesho Jumatano tarehe 26 Agosti 2020 na zitahitimishwa 27 Oktoba 2020 na siku inayofuati itakuwa ni Uchaguzi Mkuu.

1 Comment

  • Nimefurahi kuona wamepiga picha ya pamoja ,lakini wasimamizi was uchaguzi watende haki

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!