WAGOMBEA 16 wa vyama vya siasa nchini Tanzania, watachukuana kuwania Ubunge wa Arusha Mjini katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).
Wagombea hao, wameteuliwa leo Jumanne tarehe 25 Agosti 2020 na Msimamizi wa uchaguzi jimbo hilo Arusha Mjini, Dk John Pima.
Walioteuliwa ni mbunge anayetetea nafasi hiyo, Godbless Lema wa Chadema na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo anayegombea kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Leman na Gambo wanatarajia kuchuana kuwania uwakilishi wa wananchi hao wa Arusha Mjini.
Wagombe wengine ni; Zuberi Mwinyi (ADA- TADEA), Shayo John (ACT- Wazalendo), Husna Kundi(AAFP), Matayo Richard (CCK), Magdalena Shanghai (CUF), Elisante Mjema (Demokrasia Makini), Elizabeth Godfrey (DP), Epsiba Kiwhelu (NCCR- Mageuzi), Mkama Rashid(NRA), Simion Bayo(SAU), Alfred Mollel (UDP) na Elias Sumari(UPDP).
Kampeni za uchaguzi huo zinaanza kesho Jumatano tarehe 26 Agosti 2020 na zitahitimishwa 27 Oktoba 2020 na siku inayofuati itakuwa ni Uchaguzi Mkuu.
Nimefurahi kuona wamepiga picha ya pamoja ,lakini wasimamizi was uchaguzi watende haki