Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magari 10 yamfanya Dk. Mathayo wa CCM kuhojiwa Takukuru
Habari za Siasa

Magari 10 yamfanya Dk. Mathayo wa CCM kuhojiwa Takukuru

Spread the love

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Kilimanjaro imemhoji Mbunge wa Same Magharibi (CCM), Dk.Mathayo David Mathayo kwa tuhuma za kukiuka sheria za uchaguzi kwa kuingiza magari 10  maalum ya kubebea wa gonjwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro…(endelea)

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kilimanajro, Fidelis Kalungula amesema tarehe 7 Julai 2020 walipata taarifa za uingizwaji wa magari 10 katika jimbo la Same ambapo walifuatilia kwa ukaribu na kuthibitisha kuingia kwa magari hayo na kisha kuyakamata.

“Mnamo tarehe 7 mwezi huu tulipata taarifa kuna magari 10 yanakuja Kilimanjaro ambayo yanadhaniwa ni ya mbunge aliyekuwa madarakani na kwamba yamekuja kwa nia ya kuvunja sheria na makatazo yaliyopo katika sheria ya gharama za uchaguzi hivyo tulichokifanya hatua ya kwanza ili tupate ushahidi ni kuyashikilia hayo magari na mpaka sasa tunayashikilia,”amesema Kalungula

“Bado tunaendelea kuyashikilia magari hayo kwa ajili ya kupata ushahidi, kwamba je ni kweli ujio wa magari hayo yana uvunjifu wowote wa makatazo ya sheria ya Takukuru namba 11 ya mwaka 2007? tunaendelea na uchunguzi wa jambo hilo na baadhi ya watu wengine tumeshawaita watupe ufafanuzi ili kusudi siku ya mwisho tuwe na usahihi wa jambo hilo,” amesema

Aidha amesema magari hayo 10 yalikuwa yameandikwa kuonyesha yanaenda kata mbalimbali zilizopo jimboni kwa mbunge huyo hivyo wanaendelea na uchunguzi ili ukweli upatikane na kwamba hawatamwonea yoyote au kwenda kinyume na sheria inavyowaongoza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!