Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magari 10 yamfanya Dk. Mathayo wa CCM kuhojiwa Takukuru
Habari za Siasa

Magari 10 yamfanya Dk. Mathayo wa CCM kuhojiwa Takukuru

Spread the love

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Kilimanjaro imemhoji Mbunge wa Same Magharibi (CCM), Dk.Mathayo David Mathayo kwa tuhuma za kukiuka sheria za uchaguzi kwa kuingiza magari 10  maalum ya kubebea wa gonjwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro…(endelea)

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kilimanajro, Fidelis Kalungula amesema tarehe 7 Julai 2020 walipata taarifa za uingizwaji wa magari 10 katika jimbo la Same ambapo walifuatilia kwa ukaribu na kuthibitisha kuingia kwa magari hayo na kisha kuyakamata.

“Mnamo tarehe 7 mwezi huu tulipata taarifa kuna magari 10 yanakuja Kilimanjaro ambayo yanadhaniwa ni ya mbunge aliyekuwa madarakani na kwamba yamekuja kwa nia ya kuvunja sheria na makatazo yaliyopo katika sheria ya gharama za uchaguzi hivyo tulichokifanya hatua ya kwanza ili tupate ushahidi ni kuyashikilia hayo magari na mpaka sasa tunayashikilia,”amesema Kalungula

“Bado tunaendelea kuyashikilia magari hayo kwa ajili ya kupata ushahidi, kwamba je ni kweli ujio wa magari hayo yana uvunjifu wowote wa makatazo ya sheria ya Takukuru namba 11 ya mwaka 2007? tunaendelea na uchunguzi wa jambo hilo na baadhi ya watu wengine tumeshawaita watupe ufafanuzi ili kusudi siku ya mwisho tuwe na usahihi wa jambo hilo,” amesema

Aidha amesema magari hayo 10 yalikuwa yameandikwa kuonyesha yanaenda kata mbalimbali zilizopo jimboni kwa mbunge huyo hivyo wanaendelea na uchunguzi ili ukweli upatikane na kwamba hawatamwonea yoyote au kwenda kinyume na sheria inavyowaongoza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!