Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Michezo Mkude, Morrison nje mechi mbili
Michezo

Mkude, Morrison nje mechi mbili

Jonas Mkude
Spread the love

KIUNGO wa Simba, Jonas Mkude na nyota wa Yanga, Bernard Morrison wamefungiwa kucheza michezo miwili pamoja na faini ya Sh. 500,000 kwa makosa ya utovu wa nidhamu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Maamuzi hayo yametoka chini ya Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), chini ya Mwenyekiti wake, Peter Hella ambaye alisoma maamuzi hayo.

Mkude amefungiwa mara baada ya kumpiga kiwiko mchezaji wa timu ya Biashara ya Mara, kwenye mchezo wa Ligi Kuu iliyochezwa tarehe 22 Februari, 2020 kwenye Uwanja wa Taifa.

Bernard Morrison

Morrison aliingia kwenye adhabu hiyo baada ya kumpiga kiwiko mchezaji wa Tanzania Prisons kutoka Mbeya na adhabu hizo zitaanza mara moja.

Klabu hizo zitaanza kuwakosa wachezaji hao kwenye michezo ya leo ya Ligi Kuu, ambapo Simba itashuka dimbani kuikabili Mbeya City, huku Yanga watakuwa Uwanja wa Taifa, kuikaribisha Namungo FC kutoka Lindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!