Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto na wenzake waachiwa, asema…
Habari za Siasa

Zitto na wenzake waachiwa, asema…

Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi wa chama cha siasa cha upinzania nchini Tanzania cha ACT-Wazalendo na viongozi wengine waliokuwa wakishikiliwa na Polisi Mkoa wa Lindi wameachiwa kwa dhamana. Anaripoti Faki Sosi, Lindi … (endelea).

Zitto na viongozi hao walikamatwa jana Jumanne asubuhi tarehe 23 Juni 2020 wakiwa katika kikao cha ndani katika ukumbi wa Starnford Bridge, Kilwa Masoko mkoani Lindi.

Wengine ni; Mbunge wa Kilwa Kusini (CUF), Seleman Bungara maarufu ‘Bwege’ , Akida Mawanja, Mlinzi wa Zitto na Shaweji Mketo ambaye ni Mkurugenzi wa Oganaizesheni.

Pia, Swalehe Mketo aliyekuwa diwani wa CUF Kata ya Kibata, Abubakari Kama Mwenyekiti wa Jimbo Kilwa Kusini, Isihaka Mchinjika, Mwenyekiti wa Mkowa wa Lindi, na Mahadhi Mangona Katibu Mwenezi wa jimbo hilo.

Bonifancia Mapunda, wakiliwa kina Zitto amesema, uchunguzi wa tuhuma za kufanya maandamano bila kibali haujakamilika na wametakiwa kuripoti kituoni hapo tarehe 1 Juni 2020.

Mara baada ya kuachiwa, Zitto amezungumza na waandishi wa habari katika ofisi za  jimbo la Lindi Mjini ambapo amesema, kilichomtokea kinazidi kumuimarisha na wala hawezi kurudi nyuma katika mapambano ya kutetea haki za wananchi na demokrasia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!