Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CCM azichongea halmashauri bungeni
Habari za Siasa

Mbunge CCM azichongea halmashauri bungeni

Mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga
Spread the love

GOODLUCK Mlinga, Mbunge wa Ulanga kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), amezichongea halmashauri bungeni, kwamba zina tatizo kubwa la matumizi mabaya na ubadhirifu wa fedha za mapato. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mlinga ameibua tuhuma hizo wakati akiuliza swali bungeni jijini Dodoma, leo Ijumaa tarehe 12 Juni 2020. Katika swali lake, Mlinga amehoji Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hilo.

“Kumekuwa na tatizo kubwa la matumizi mabaya na ubadhirifu wa fedha za mapato ya ndani pamoja na ruzuku katika Halmshauri nyingi nchini, je, Serikali imejipanga vipi kukabiliana na tatizo hili,” amehoji Mlinga.

Akijibu swali hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, amesema Serikali imeboresha mfumo wa ukusanyaji mapato na matumizi, ili kukabiliana na tatizo hilo.

“Katika kukabiliana na ubadhilifu wa fedha kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa, Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo, kuboresha mfumo wa ukusanyaji mapato na mifumo ya matumizi (Epicor 10.02 na FFARS) ili kudhibiti ubadhilifu wakati wa makusanyo na wakati wa matumizi,” amesema.

Waziri huyo mwenye dhamana ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, amesema katika mwaka wa fedha wa 2018/2019, Serikali ilizipatia halmashauri zote nchini, mashine bora na za kisasa za kielektroniki kwa ajili ya kukusanya mapato.

Aidha, amesema Serikali  imeimarisha mfumo wa ukaguzi wa ndani kuanzia ngazi ya Halmashauri, pia inatoa ushirikiano wa kutosha kwa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ili kumuwezesha kufanya kazi yake kikamilifu.

“Serikali pia imekuwa ikichukua hatua za kinidhamu na kisheria kwa watumishi wote wanaobainika kuhusika kwenye ubadhilifu wa fedha za Umma,” amesema Waziri wa Tamisemi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!