Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba yaonyesha umwamba kuelekea Ligi Kuu
Michezo

Simba yaonyesha umwamba kuelekea Ligi Kuu

Spread the love

KLABU ya Simba leo imeibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Transit Camp kwenye mchezo wa kujipima nguvu kuelekea kuendelea na michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajia kuanza juni 13, 2020. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam…(endelea).

Katika mchezo huo magoli ya Simba yalifungwa na Deo Kanda (3), Gerson Fraga (15), Tairone Santos (17) na bao la mwisho lilifungwa na mshambuliaji wao kinara Meddie Kagere (46), huku upande wa Transit Camp mabao yao yalifungwa na Hamadi Habibu (45+1) na Nisile Kisimba (64).

Baada ya mchezo huo Simba inatarajia kushuka dimbani siku ya Jumapili kuwakabili Ruvu Shooting, kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam katika muendelezo wa mchezo wa Ligi Kuu.

Simba mpaka sasa ndio vinara kwenye msimamo wa Ligi hiyo baada ya kujikusanyia alama 72, toka Ligi hiyo ilivyosimama Machi mwaka huu kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Corona (Covid-19).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!