Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Michezo Simba yaonyesha umwamba kuelekea Ligi Kuu
Michezo

Simba yaonyesha umwamba kuelekea Ligi Kuu

Spread the love

KLABU ya Simba leo imeibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Transit Camp kwenye mchezo wa kujipima nguvu kuelekea kuendelea na michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajia kuanza juni 13, 2020. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam…(endelea).

Katika mchezo huo magoli ya Simba yalifungwa na Deo Kanda (3), Gerson Fraga (15), Tairone Santos (17) na bao la mwisho lilifungwa na mshambuliaji wao kinara Meddie Kagere (46), huku upande wa Transit Camp mabao yao yalifungwa na Hamadi Habibu (45+1) na Nisile Kisimba (64).

Baada ya mchezo huo Simba inatarajia kushuka dimbani siku ya Jumapili kuwakabili Ruvu Shooting, kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam katika muendelezo wa mchezo wa Ligi Kuu.

Simba mpaka sasa ndio vinara kwenye msimamo wa Ligi hiyo baada ya kujikusanyia alama 72, toka Ligi hiyo ilivyosimama Machi mwaka huu kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Corona (Covid-19).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Mwana FA anogesha Tamasha la Exim Bima Festival

Spread the loveNAIBU Waziri Wa Utamaduni, Sanaa Na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana...

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

error: Content is protected !!