Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Simba yaonyesha umwamba kuelekea Ligi Kuu
Michezo

Simba yaonyesha umwamba kuelekea Ligi Kuu

Spread the love

KLABU ya Simba leo imeibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Transit Camp kwenye mchezo wa kujipima nguvu kuelekea kuendelea na michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara inayotarajia kuanza juni 13, 2020. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam…(endelea).

Katika mchezo huo magoli ya Simba yalifungwa na Deo Kanda (3), Gerson Fraga (15), Tairone Santos (17) na bao la mwisho lilifungwa na mshambuliaji wao kinara Meddie Kagere (46), huku upande wa Transit Camp mabao yao yalifungwa na Hamadi Habibu (45+1) na Nisile Kisimba (64).

Baada ya mchezo huo Simba inatarajia kushuka dimbani siku ya Jumapili kuwakabili Ruvu Shooting, kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam katika muendelezo wa mchezo wa Ligi Kuu.

Simba mpaka sasa ndio vinara kwenye msimamo wa Ligi hiyo baada ya kujikusanyia alama 72, toka Ligi hiyo ilivyosimama Machi mwaka huu kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Corona (Covid-19).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!