Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Amuua mama yake, anywa damu yake
Habari Mchanganyiko

Amuua mama yake, anywa damu yake

Spread the love

DANIEL Emanuel (32), mkazi wa Arusha, Sakila katika Wilaya ya Arumeru, amekuta akinywa damu ya mama yake Eliyamulika Emmanuel Sarakikya (79) baada ya kumuua. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Taarifa zinaeleza, Daniel alimuua mama yake kwa shoka na kisha akatenganisha, kichwa, mkono, miguu na kiwiliwili chake, akakinga damu ya mama yake kwenye kikombe na kunywa.

Akizungumzia tukio hilo Jonathan Shana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha amesema, mauaji ya mama huyo yamefanywa saa 9 alasiri tarehe 15 Mei 2020, katika Kijiji cha Sakila, Kata ya Kikatiti, King’ori wilayani Arumeru.

Kamanda Shana amesema, wakati Daniel akifanya tukio hilo, majirani walishuhudia akinywa damu ya mama yake baada ya kumuua.

“Daniel alimkata mama yake kwa shoka shingoni na kisha kutenganisha na kiwiliwili chake. Akaona haitoshi, akaanza kukata mguu wa kulia, akakata wa mguu wa kushoto na mkono. Wakati anafanya unyama huu, alikuwa anakinga damu kwenye kikombe anakunywa,” amesema.

Amesema, polisi walipopata taarifa kutoka kwa majirani, walifika haraka kwenye eneo la tukio na kumkuta Daniel akiendelea kunywa damu, na alipowaona alijaribu kukimbia.

“Alipotuona alijaribu kukimbia lakini tulifanikiwa kumkamata,” amesema Kamnda Shana na kuongeza “tumemweka mahabusu hadi upelelezi utakapokamilika.”

Amesema, taarifa za awali zinadai, Daniel ana matatizo ya akili. Licha ya taarifa hizo za awali kutoka kwa baadhi ya watu, Kamanda Shana ametilia mashaka hasa akizungatia maandalizi yaliyofanywa na Danile kabla ya mauaji.

“Hili sikubaliani sana sababu aliwezaje kuandaa shoka, mazingira tulivu yasio na watu pia kwanini kama hana akili alikimbia polisi alipowaona,” amehoji.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!