Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Corona sasa yamkumba mbunge wa Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Corona sasa yamkumba mbunge wa Tanzania

Spread the love

NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri, Dk. Tulia Akson, amelitangazia Bunge kuwa mmoja wa wabunge wa Bunge hilo, amepatwa na virusi vya Corona. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea). 

Akizungumza bungeni mchana huu, muda mfupi kabla ya kughairisha Bunge, Dk. Tulia alisema, mbunge huyo alithibitika kuwa na ugonjwa huo, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Naibu Spika Tulia, hakutaja jina la mbunge ambaye amesema ameambukizwa virusi hivyo.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge wamemwambia mwandishi wa habari hizi kuwa mbunge huyo anatokea moja ya majimbo ya mkoa wa Dar es Salaam.

Alisema, “tumepata taarifa kuwa mbunge mwenzetu alikuja Dodoma kutokea Dar es Salaam, Jumatano iliyopita. Akiwa hapa Dodoma akaanza kujisikia vibaya na hivyo akalazimika kurudi Dar es Salaam

“Alipofika Dar es Salaam akaenda hospitali ambako baada ya kufanyiwa uchunguzi na madaktari bingwa wanaojihusisha na ugonjwa huu, amethibitika kuwa na maambukizi.”

Dk. Tulia alitoa tangazo hilo, wakati akighairisha Bunge kupisha msiba wa mbunge wa Viti Maalum (CCM), Gerturde Pangalile Rwakatare.

Mbunge Rwakatare ambaye ni Askofu wa Kanisa la Assembliess of God – maarufu kama Mlima wa Moto – alikutwa na mauti asubuhi ya kuamkia leo Jumatatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!