Sunday , 3 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Corona sasa yamkumba mbunge wa Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Corona sasa yamkumba mbunge wa Tanzania

Spread the love

NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri, Dk. Tulia Akson, amelitangazia Bunge kuwa mmoja wa wabunge wa Bunge hilo, amepatwa na virusi vya Corona. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea). 

Akizungumza bungeni mchana huu, muda mfupi kabla ya kughairisha Bunge, Dk. Tulia alisema, mbunge huyo alithibitika kuwa na ugonjwa huo, mwishoni mwa wiki iliyopita.

Naibu Spika Tulia, hakutaja jina la mbunge ambaye amesema ameambukizwa virusi hivyo.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge wamemwambia mwandishi wa habari hizi kuwa mbunge huyo anatokea moja ya majimbo ya mkoa wa Dar es Salaam.

Alisema, “tumepata taarifa kuwa mbunge mwenzetu alikuja Dodoma kutokea Dar es Salaam, Jumatano iliyopita. Akiwa hapa Dodoma akaanza kujisikia vibaya na hivyo akalazimika kurudi Dar es Salaam

“Alipofika Dar es Salaam akaenda hospitali ambako baada ya kufanyiwa uchunguzi na madaktari bingwa wanaojihusisha na ugonjwa huu, amethibitika kuwa na maambukizi.”

Dk. Tulia alitoa tangazo hilo, wakati akighairisha Bunge kupisha msiba wa mbunge wa Viti Maalum (CCM), Gerturde Pangalile Rwakatare.

Mbunge Rwakatare ambaye ni Askofu wa Kanisa la Assembliess of God – maarufu kama Mlima wa Moto – alikutwa na mauti asubuhi ya kuamkia leo Jumatatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

Habari za Siasa

Dk. Biteko aagiza wakurugenzi TANESCO kukemea rushwa kwenye maeneo yao

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Uongozi wa Samia kuendelea hadi 2030

Spread the loveKWETU sisi tuliowahi kusoma sekondari, iwe O levo au A...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Bado askari wastaafu wanaonewa

Spread the loveRAIS wangu Samia Suluhu Hassan tunaendelea kumshukuru Mungu kwamba wote...

error: Content is protected !!