Wednesday , 1 May 2024
Home Kitengo Michezo Wakorea kuwapiga tafu TFF kuinua soka la Vijana
Michezo

Wakorea kuwapiga tafu TFF kuinua soka la Vijana

Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF$, leo imengia makubariano na Shirika la Maendeleo nchini Korea (KIDC) kwa ajili ya maendeleo ya mpira wa miguu wa vijana kwa wanawake kwa kuleta wakufunzi katika kipindi cha miaka miwili. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Katika makubaliano hayo KIDC italeta wataalamu wapatao 30 katika shule zilizopo kwenye mkoa wa Dar es Salaam ambazo ni Fountain gate, Jangwani, Kibasila, Chang’ombe na Benjamini Mkapa katika kipindi cha mwaka mmoja na baadae kuendelea katika mikoa mingine.

Baada ya makubaliano hayo Rais wa TFF Wallace Karia alieleza kuwa wanaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kufanikisha malengo kwenye soka la wanawake kwa kuwa bajeti yao ni ndogo ili kufanikisha kucheza kombe la dunia lililo mbele.

“Makubaliano haya tunaingia leo ni ya miaka miwili ambapo KIDC kufikia mwezi Disemba mpaka juni watakuwa wameleta wataalamu 30 kwa ajili ya kuendeleza program hiyo ambapo itaanza katika baadhi ya shule kwenye mkoa wa Dar es Salaam,” alisema Karia.

Katika hatua nyingine Karia amesema kuwa kwenye mkataba huo pia TFF itafaidika kwa kupata wataalamu watatu ambao wawili watakuwa ndani ya idara ya habari na mmoja kwenye idara ya ufundi katika kipindi cha mwaka mmoja. 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!