Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dovutwa ang’olewa UPDP 
Habari za Siasa

Dovutwa ang’olewa UPDP 

Fahmi Dovutwa, aliyekuwa Mwenyekiti wa UPDP
Spread the love

FAHMI Dovutwa, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha UPDP, ameondolewa kwenye nafasi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Imeelezwa, Dovutwa ameng’olewa kwenye nafasi hiyo kwa madai, alikitoa chama hicho katika kushiriki wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, uliofanyika tarehe 24 Novemba 2019.

Kwa mujibu wa Abdalla Mohammed Khamis, Kaimu Mwenyekiti wa UPDP,  Dovutwa amevuliwa uenyekiti na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.

Khamis amesema Dovutwa amepewa adhabu hiyo kufuatia hatua yake ya kutangaza UPDP hakitashiriki uchaguzi huo, pasina kupewa ridhaa na uongozi wa chama hicho.

Ameeleza kuwa, kitendo hicho ni kinyume na katiba ya UPDP, pia, kimesababisha chama hicho kukosa wenyeviti wa serikali za mitaa.

Uchaguzi wa serikali za mitaa ulifanyika pasina ushiriki wa vyama vya upinzani nane, ikiwemo chama cha UPDP.

Vyama hivyo, vilisusa kushiriki uchaguzi huo kwa madai kuwa, mchakato wake ulikiuka kanuni za uchaguzi huo.

 

 

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!