Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa M/Kiti BAVICHA afunguliwa kesi ya uhujumu uchumi
Habari za Siasa

M/Kiti BAVICHA afunguliwa kesi ya uhujumu uchumi

Spread the love

AYUBU Sikagonamo, Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA), Mkoa wa Songwe amefutiwa kesi ya kukutwa na silaha, na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na BAVICHA kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, Sikagonamo amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Momba leo tarehe 18 Septemba 2019 na kubadilishiwa shitaka.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Sikagonamo alifikishwa mahakamani hapo na kufutiwa kesi ya awali ya kukutwa na silaha, kisha kukamatwa tena na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi Namba 10 ya mwaka 2019.

Taarifa hiyo ya BAVICHA inaeleza, kesi hiyo itaanza kusikilizwa tarehe 2 Oktoba 2019.

Sikagonamo alikamatwa na Jeshi la Polisi Julai mwaka huu, akituhumiwa kukutwa na silaha nyumbani kwake eneo la Mwaka katika Kata ya Chipaka, Tunduma mkoani Songwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!