Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Jengo Old Tanga Sekondari lateketea
Habari Mchanganyiko

Jengo Old Tanga Sekondari lateketea

Spread the love

JENGO moja la Shule ya Sekondari ya Old Tanga, iliyoko jijini Tanga limeteketea kwa moto mchana wa leo tarehe 18 Septemba 2019. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Tukio hilo limethibitishwa na Edward Bukombe, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Tanga, aliyesema kwamba moto huo ulizuka majira ya saa 6.00 mchana.

Kamanda Bukombe amesema, hadi sasa chanzo cha moto huo bado hakijajulikana. Hata hivyo, amesema moto huo haujaleta madhara.

“Kuna jengo moja ambalo ni ukumbi, ni jengo la zamani tangu enzi ya mkoloni limeungua lote kwa moto. Bado hatujajua chanzo chake. Lakini haujaleta madhara yoyote kwa binadamu,” amesema Kamanda Bukombe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!