Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa M/Kiti BAVICHA afunguliwa kesi ya uhujumu uchumi
Habari za Siasa

M/Kiti BAVICHA afunguliwa kesi ya uhujumu uchumi

Spread the love

AYUBU Sikagonamo, Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA), Mkoa wa Songwe amefutiwa kesi ya kukutwa na silaha, na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na BAVICHA kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter, Sikagonamo amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Momba leo tarehe 18 Septemba 2019 na kubadilishiwa shitaka.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Sikagonamo alifikishwa mahakamani hapo na kufutiwa kesi ya awali ya kukutwa na silaha, kisha kukamatwa tena na kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi Namba 10 ya mwaka 2019.

Taarifa hiyo ya BAVICHA inaeleza, kesi hiyo itaanza kusikilizwa tarehe 2 Oktoba 2019.

Sikagonamo alikamatwa na Jeshi la Polisi Julai mwaka huu, akituhumiwa kukutwa na silaha nyumbani kwake eneo la Mwaka katika Kata ya Chipaka, Tunduma mkoani Songwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!