Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Airbus A220-300 iliyokamatwa Afrika Kusini yatua Tanzania
Habari za SiasaTangulizi

Airbus A220-300 iliyokamatwa Afrika Kusini yatua Tanzania

Spread the love

NDEGE ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), iliyokuwa imeshikiliwa nchini Afrika Kusini, tayari imetua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ndege hiyo iliyokuwa imeshikiliwa kwa amri ya Mahakama Kuu ya Gauteng, Johannesburg imewasili JNIA tarehe 4 Septemba 2019 saa 2:25 usiku.

Kushikiliwa kwa ndege hiyo kulitokana na kesi ya fidia iliyofunguliwa mahakamani hapo na Hermanus Steyn dhidi ya Serikali ya Tanzania.

Katika kesi hiyo, raia huyo wa Afrika Kusini alieleza kuwa anaidai serikali ya Tanzania malipo yaliyobaki ya fidia ya mali zake zilizotaifishwa mwaka 1982.

Akipokea ndege hiyo JNIA, Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje alieleza furaha yake ambapo alisema, “Ni faraja kwa nchi kushinda kesi.”

Prof. Kabudi amewapongeza majaji wa Afrika Kusini kusimamia haki uliowezesha ndehe hiyo kuachwa huru na kurejea nchini. Hata hivyo ameeleza kutokuwa na wasiwasi wowote kwa ndege za Tanzania kukamatwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!