Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Palestina yawalilia waliopoteza maisha ajali ya moto Morogoro 
Habari Mchanganyiko

Palestina yawalilia waliopoteza maisha ajali ya moto Morogoro 

Lori la mafuta likiteketea kwa moto na kusababisha baadhi ya watu kuungua moto
Spread the love

NCHI ya Palestina imetoa pole kwa serikali ya Tanzania kufuatia vifo vya watu 93 vilivyotokea katika ajali ya mlipuko wa tenki la mafuta mkoani Morogoro tarehe 10 Agosti 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Salamu hizo za pole zimetolewa na Dk. Riad Malki Waziri wa Mambo ya nje wa Palestina kupitia barua aliyomwandikia Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana tarehe 16 Agosti 2019 na Kitengo cha Mawasiliano cha Ubalozi wa Palestina hapa nchini,  Dk. Malki ameeleza kuhuzunishwa na tukio hilo, huku akisema kwamba serikali na raia wa Palestina wanawaombea majeruhi wote wapone haraka pamoja na marehemu wapumzike kwa amani.

“Nimepokea kwa huzuni kubwa habari za kifo na majeruhi ya raia kutokana na tukio la mlipuko wa tanki la mafuta lililotokea mkoa wa Morogoro. Kwa niaba ya serikali na watu wa nchi ya Palestina, ningependa kutoa salamu zangu za pole kwa watu na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mawazo yetu na sala ziko pamoja na familia za waathirika wa mlipuko huo na kuwaombea majeruhi wapone haraka,” inaeleza sehemu ya barua ya Dk. Malki kwa Prof. Kabudi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

error: Content is protected !!