Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Palestina yawalilia waliopoteza maisha ajali ya moto Morogoro 
Habari Mchanganyiko

Palestina yawalilia waliopoteza maisha ajali ya moto Morogoro 

Lori la mafuta likiteketea kwa moto na kusababisha baadhi ya watu kuungua moto
Spread the love

NCHI ya Palestina imetoa pole kwa serikali ya Tanzania kufuatia vifo vya watu 93 vilivyotokea katika ajali ya mlipuko wa tenki la mafuta mkoani Morogoro tarehe 10 Agosti 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Salamu hizo za pole zimetolewa na Dk. Riad Malki Waziri wa Mambo ya nje wa Palestina kupitia barua aliyomwandikia Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana tarehe 16 Agosti 2019 na Kitengo cha Mawasiliano cha Ubalozi wa Palestina hapa nchini,  Dk. Malki ameeleza kuhuzunishwa na tukio hilo, huku akisema kwamba serikali na raia wa Palestina wanawaombea majeruhi wote wapone haraka pamoja na marehemu wapumzike kwa amani.

“Nimepokea kwa huzuni kubwa habari za kifo na majeruhi ya raia kutokana na tukio la mlipuko wa tanki la mafuta lililotokea mkoa wa Morogoro. Kwa niaba ya serikali na watu wa nchi ya Palestina, ningependa kutoa salamu zangu za pole kwa watu na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mawazo yetu na sala ziko pamoja na familia za waathirika wa mlipuko huo na kuwaombea majeruhi wapone haraka,” inaeleza sehemu ya barua ya Dk. Malki kwa Prof. Kabudi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!