Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Membe, Musiba kukutana Julai 2
Habari Mchanganyiko

Membe, Musiba kukutana Julai 2

Spread the love

MAKAHAMA Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam imepanga tarehe 2 Julai 2019 kutoa uamuzi wa madai ya fidia ya Sh. 10 bilioni, ya kesi iliyofunguliwa na Bernard Membe, waziri wa zamani wa Mambo ya Nje dhidi ya Cyprian Musiba. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).  

Mahakama hiyo mbele ya Jaji Jocqwine Demela leo tarehe 17 Mei 2019, imepanga tarehe hiyo baada ya mawakili wa pande zote mbili,  Wakili Majura Magafu anamtetea Musiba na Wakili Johnathan Mndeme anayemwakilisha Membe, kusikilizwa hoja zao.

Upande wa walalamikiwa uliwasilisha maombi namna 119/2019 ya kuomba kuongezewa muda wa kuwasilisha majibu yake nje ya muda.

Katika kesi hiyo Musiba, anayejitambulisha kama mwanaharakati na mtetezi wa Serikali na Rais John Magufuli, anatuhumiwa na Membe kwamba, anamhujumu Rais Magufuli, ikiwa ni pamoja na kufanya kampeni za kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!