Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Taratibu za kimila zatumika kutafuta wauaji
Habari Mchanganyiko

Taratibu za kimila zatumika kutafuta wauaji

Maelfu ya wakati wa Karatu wakiwa katika mazishi ya Afisa Elimu Maalum wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu, Martin Goi (picha ndogo)
Spread the love

MAELFU ya wananchi wameshiriki katika mazishi ya Afisa Elimu Maalum wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu, Martin Goi, aliyeuawa kwa kupigwa risasi na wanaoitwa na serikali, “watu wasiojulikana.” Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Goi alipigwa risasi tarehe 15 Januari mwaka huu, katika mgahawa wa Rhotian Glades, wilayani Karatu, majira ya saa tatu usiku. Goi alizaliwa katika kijiji cha Dofa wilayani Karatu.

Taarifa zinasema, mara baada ya shambulio hilo na kabla mauti kumfika, Goi alipelekwa kwenye hospitali ya Sanawati mkoani Arusha. Alifia katika hospitali hiyo siku mbili baada ya kushambuliwa.

Kwa mujibu wa habari hizo, mara baada ya marehemu Goi kuzikwa, wananchi kadhaa walishiriki katika maombi maalum ya kumtambua waliofanya mauaji hayo.

Maombi hayo yalihitimishwa jana tarehe 22 Januari kwa dua na sala za kimila na kidini. Kwa kawaida, maombi ya aina hiyo hujibu katika kipindi kifupi cha wiki moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!