Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Mbao FC waitoa nishai Gor Mahia
Michezo

Mbao FC waitoa nishai Gor Mahia

Spread the love

KLABU ya Mbao FC imefanikiwa kuiondoa timu ya FC Gor Mahia kutoka Kenya kwenye michuano ya kombe la Sport Pesa kwa njia ya mikwaji ya penalti 4-3 baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika dakika 90 za mchezo hivyo nakufanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea)

Gor Mahia ambao walikuwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo kwa miaka miwili mfululizo ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Oriech dakika ya  56, na baadae Mbao wakafanikiwa kusawazisha dakika ya 76 kupitia Aboubakar Ngalema.

Baada ya ushindi huo Mbao FC  itakutana na Kariobang Sharks kutoka Kenya katika mchezo wa nusu fainali siku ya Ijumaa.

Ikumbukwe bingwa wa michuano hiyo atapata zawadi ya kombe na kiasi cha fedha Sh. 30 milioni sambamba na kucheza mechi na klabu ya Evarton FC inayoshiliki Ligi Kuu nchini England mwezi Julai mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!