Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mahakama yaigeukia Serikali kesi ya kina Kitilya
Habari Mchanganyiko

Mahakama yaigeukia Serikali kesi ya kina Kitilya

Spread the love

MAHAKAMA ya hakimu Mkazi Kisutu imeutaka upande wa Jamhuri kuharakakisha upelelezi wa kesi inayomkabili Kamishna wa zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya na wenzake wawili wanaokabiliwa na kesi ya kutakatisha fedha wanaendelea kusota rumande kutokana na upelelezi wa kesi yao kutokamilika. Anaripoti Faki Sosi …(endelea).

Huruma shahahi Hakimu Mkuu katika Mahakama hiyo ameutaka upande huo mara baada ya Wakili wa Serikali Mkuu Kishenyi Mutalemwa kudai kuwa kesi hiyo imeitwa kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi unakaribia kuifika ukingoni kukamilika.

Washatakiwa wengine kwenye kesi hiyo ni pamoja na Shose Sinare aliyekuwa Miss Tanzania (1996) na Ofisa wa Benki ya Stanbic, Sioi Solomon.

Wakili wa utetezi Alex Mgongolwa alihoji ni ukingo gani huo ambao unazungumziwa na upande wa mashtaka.

Hakimu shahidi ameahirisha kesi hiyo hadi Novemba 30, mwaka huu na kuusisitiza upande wa mashtaka kufanya jitihada kukamilisha upelelezi.

Washtakiwa hao kwa pamoja  wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha ambapo Machi 2013 jijini Dar es Salaam walijipatia Dola za Marekani milioni sita, wakionyesha kuwa fedha hizo zilikuwa ni malipo ya ada ya uwezeshaji upatikanaji wa mkopo  na zililipwa kupitia  Kampuni ya Egma T Ltd.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

error: Content is protected !!