Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko India wapiga marufuku kuacha mke
Habari Mchanganyiko

India wapiga marufuku kuacha mke

Spread the love

SERIKALI ya India imeanza utekelezaji wa muswada wa sheria ya ulinzi wa haki katika Ndoa wa mwaka 2017 uliokwama kupitishwa na bunge la nchi hiyo, ambao unalenga kuwabana wanaume wa kiislamu kutoa talaka tatu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Muswada huo ambao unatafisri utolewaji wa talaka tatu za papo kwa papo kama kosa la jinai ambapo mhusika anaweza kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela, ulikwama kupitishwa bungeni mwezi Agosti 2018 baada ya pande zote mbili (upinzani na serikali) kukosa makubaliano.

Muswada huo uliowasilishwa bungeni na serikali ya Narendra Modi ulikwama kupitishwa kutokana na kutopigiwa kura na wabunge wengi.

Akizungumza na wanahabari jana Waziri wa Sheria India, Ravi Shankar Prasad alisema serikali ya nchi hiyo imeamua kuanza utekelezaji wa sheria hiyo baada ya kukithiri kwa matukio ya utolewaji wa talaka hizo licha ya maamuzi yaliyotolewa na mahakama kuu ya nchi hiyo kuhusu usitishaji wa talaka hizo kutokana na kuwa kinyume na katiba ya India.

Hata hivyo, Vyama vya Upinzani India vimekosoa vikali uamuzi huo vikidai kuwa, baadhi ya masharti yaliyomo katika muswada huo ni magumu kutekelezeka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!