Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kesi ya kuvunja Muungano yakwama
Habari Mchanganyiko

Kesi ya kuvunja Muungano yakwama

Spread the love

MAHAKAMA ya Afrika Mashariki (EACJ) imetupilia mbali kesi iliyofunguliwa na wananchi ya kupinga Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Uamuzi wa kesi hiyo iliyofunguliwa na Wanzanibar 40,000 wakiongozwa na Rashid Salum Adiy,  umetolewa jana tarehe 19 Septemba 2018 na mahakama ya EACJ.

Hata hivyo, jopo la majaji watano wakiongozwa na Jaji Kiongozi, Monica Mugenyi akiwa na majaji Fakihi Jundu na Dk. Charles Nyawelo waliokuwa wanasikiliza kesi hiyo, waliwashauri walalamikaji kuwasilisha madai yao katika mahakama za Zanzibar.

Katika kesi hiyo, wajibu maombi walikuwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo upande huo ulitetewa na Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!