Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kesi ya kuvunja Muungano yakwama
Habari Mchanganyiko

Kesi ya kuvunja Muungano yakwama

Spread the love

MAHAKAMA ya Afrika Mashariki (EACJ) imetupilia mbali kesi iliyofunguliwa na wananchi ya kupinga Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Uamuzi wa kesi hiyo iliyofunguliwa na Wanzanibar 40,000 wakiongozwa na Rashid Salum Adiy,  umetolewa jana tarehe 19 Septemba 2018 na mahakama ya EACJ.

Hata hivyo, jopo la majaji watano wakiongozwa na Jaji Kiongozi, Monica Mugenyi akiwa na majaji Fakihi Jundu na Dk. Charles Nyawelo waliokuwa wanasikiliza kesi hiyo, waliwashauri walalamikaji kuwasilisha madai yao katika mahakama za Zanzibar.

Katika kesi hiyo, wajibu maombi walikuwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo upande huo ulitetewa na Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Ditopile aungana na Wana-Kongwa kwa Iftar, wamuombea dua Rais Samia

Spread the loveKATIKA muendelezo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, Mbunge wa Viti...

Habari Mchanganyiko

PSSSF yawekeza kwenye viwanda 4, kuzalisha ajira 3,000

Spread the loveKATIKA kuisaidia Serikali kupunguza tatizo la uhaba wa ajira nchini,...

Habari Mchanganyiko

Luhemeja ahimiza utunzaji rasilimali maji kwa faida ya vizazi vijavyo

Spread the love  NAIBU Katibu Mkuu, Wizara ya Maji Mhandisi Cyprian Luhemeja...

Habari Mchanganyiko

NSSF yawapa darasa wahariri uwekezaji wa nyumba, yapewa cheti

Spread the loveMFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetoa wito...

error: Content is protected !!