Saturday , 4 May 2024
Home Habari Mchanganyiko IGP Sirro afanya mabadiliko makamanda wa mikoa
Habari Mchanganyiko

IGP Sirro afanya mabadiliko makamanda wa mikoa

Hassan Nassir, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kusini Pemba
Spread the love

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amefanya mabadiliko ya baadhi ya makamanda wa polisi wa mikoa nchini, kwa kumhamisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Hassan Nassir kuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kusini Pemba. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Taarifa hiyo ya mabadiliko imetolewa leo tarehe 3 Septemba, 2018 na Msemaji waJeshi la Polisi Makao Makuu, ACP Barnabas Mwakalukwa.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, nafasi ya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, SACP Nassir imechukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba, SACP Mohamed Shehan Mohamed.

“Pia, uhamisho huo ni mabadiliko ya kawaida yanayotokea ndani ya jeshi la polisi katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi. Lengo kuu ni kufanya mabadiliko yenye tija kwa umma katika masuala ya ulinzi na usalama,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!