Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Michezo Amunike kuwapa nafasi nyingine nyota wa Simba
Michezo

Amunike kuwapa nafasi nyingine nyota wa Simba

Clifford Ndimbo, Msemaji wa TFF (kulia) akiwa na Msemaji wa Simba, Haji Manara
Spread the love

KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars, Emmanuel Amunike  ametoa msamaha kwa wachezaji wa watano wa Simba na mmoja wa Yanga aliowaondoka katika kikosi chake baada ya kuchelewa kuripoti kambini. Anaripoti Halidi Mhina …. (endelea).

Wachezaji walioondolewa katika kikosi cha Amunike ni Faisal Salum wa Yanga, Shiza Kichuya, Johhn Bocco, Hassan Dilunga, Shomari Kapombe, Jonas Mkude pamoja na Erasto Nyoni wote hao kutoka Simba.

Msemaji wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Clifford Ndimbo, amesema tatizo kazi ya wachezaji hao na Kocha Amunike limemalizika baada ya kocha huyo kukutana na nyota hao na ameahidi atawapa nafasi nyingine ya kujiunga na kikosi chake kama wataonesha tena kiwango kizuri kwenye klabu zao.

Lakini pamoja na msamaha huo nyota hao hawatajumuishwa kwenye kikosi kitakacho kwenda kuwavaa timu ya Taifa ya Uganda kwenye mchezo wa kufuzu kwa fainali za kombe la mataifa Afrika ‘AFCON’ unaotarajiwa kuchezwa Septemba 8, 2018 kwenye uwanja wa Nelson Mandela uliopo Nambole.

Naye Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema kuwa Simba hawana tofauti yoyote na kocha wala uongozi wa TFF kwa kilichotokea na kudai kuwa wameweka silaha chini na wote wanashirikiana kuiunga mkono timu ya Taifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!