Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Amunike kuwapa nafasi nyingine nyota wa Simba
Michezo

Amunike kuwapa nafasi nyingine nyota wa Simba

Clifford Ndimbo, Msemaji wa TFF (kulia) akiwa na Msemaji wa Simba, Haji Manara
Spread the love

KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars, Emmanuel Amunike  ametoa msamaha kwa wachezaji wa watano wa Simba na mmoja wa Yanga aliowaondoka katika kikosi chake baada ya kuchelewa kuripoti kambini. Anaripoti Halidi Mhina …. (endelea).

Wachezaji walioondolewa katika kikosi cha Amunike ni Faisal Salum wa Yanga, Shiza Kichuya, Johhn Bocco, Hassan Dilunga, Shomari Kapombe, Jonas Mkude pamoja na Erasto Nyoni wote hao kutoka Simba.

Msemaji wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Clifford Ndimbo, amesema tatizo kazi ya wachezaji hao na Kocha Amunike limemalizika baada ya kocha huyo kukutana na nyota hao na ameahidi atawapa nafasi nyingine ya kujiunga na kikosi chake kama wataonesha tena kiwango kizuri kwenye klabu zao.

Lakini pamoja na msamaha huo nyota hao hawatajumuishwa kwenye kikosi kitakacho kwenda kuwavaa timu ya Taifa ya Uganda kwenye mchezo wa kufuzu kwa fainali za kombe la mataifa Afrika ‘AFCON’ unaotarajiwa kuchezwa Septemba 8, 2018 kwenye uwanja wa Nelson Mandela uliopo Nambole.

Naye Msemaji wa Simba, Haji Manara amesema kuwa Simba hawana tofauti yoyote na kocha wala uongozi wa TFF kwa kilichotokea na kudai kuwa wameweka silaha chini na wote wanashirikiana kuiunga mkono timu ya Taifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!