Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli hapendi hamahama za wabunge, madiwani
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli hapendi hamahama za wabunge, madiwani

Spread the love

WIMBI la hamahama ya madiwani na wabunge wa upinzani nchini limelalamikiwa kuwa linaipeleka nchi kwenye giza la uchumi kutokana na kuingia kwenye gharama za uchaguzi zisizo na umuhimu. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Baadhi ya wabunge na madiwani wa upinzani wamekuwa wakihama vyama vyao kwa madai kuwa wanaunga mkono juhudu za Rais John Magufuli.

Akizungumza na vyombo vya habari leo tarehe 31 Agosti, 2018, Deus Kibamba, Mtafiti wa Jukwaa la Katiba Nchini (JUKATA) amesema kujiuzulu kwa wabunge na madiwani nchini, kunakinzana na jitihada za Rais Magufuli za Tanzania ya viwanda.

Kibamba amesema kuwa, Rais Magufuli hafurahishishwi na vitendo hivi vinavyoigharimu nchi kutokana na marudio ya uchaguzi unaofanyika kila wanasiasa wanapojiuzulu.

Amesema kuwa JUKATA imetoa mapendekezo ya sheria itakayodhibiti vitendo hivi na kuikomboa nchi kwenye shambulio la kiuchumi lililopitia mlango wa kisiasa.

Moja ya mapendekezo hayo ni kutorejea uchaguzi kwa diwani au mbunge atakayejivua nafasi yake ndani ya chama na kuhamia chama kingine na kurejea kugombea kwa chama alichohamia kama inavyofanywa sasa.

Mapendekezo hayo yamehalarisha uchaguzi kurejewa kwa jimbo au kata ya diwani au mbunge aliyefariki pekee.

Kibamba amesema kuwa mapendekezo hayo wanayapeleka bungeni yajadiliwe kisha kwa wananchi ili kuikomboa nchi kwenye gharama zenye kiitia hasara nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!