Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwijage: Zalisheni mbegu za kunukia kuvutia soko
Habari Mchanganyiko

Mwijage: Zalisheni mbegu za kunukia kuvutia soko

Shamba la mpunga
Shamba la mpunga
Spread the love

WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Masoko Charles Mwijage amewataka wazalishaji wa mbegu ya Mpunga zinazotoa  harufu ya kunukia aina ya Aroma kuongeza uzalishaji huku wakizingatia ubora wa harufu ya mpunga huo ili kuvutia katika soko. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Waziri Mwijage amesema hayo wakati alipotembelea banda la Maonesho la Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Nchini (TARI) lililopo kwenye uwanja wa Maonesho ya Kilimo 88 kanda ya mashariki kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere vilivyopo eneo la Tungi nje kidogo ya Manispaa ya Morogoro.

Mwijage amesema, mbegu hiyo ni nzuri na inanukia lakini upatikanaji wake umekuwa mdogo tofauti na mbegu zingine na hivyo kumfanya mkulima kuendelea kutumia mbegu zingine ambazo hazina harufu nzuri kama ya mpunga aina ya Aroma.

Akizungumzia hilo Mtafiti wa Kilimo ambaye pia ni Ofisa Mfawidhi –TARI- Dakawa Dk. Charles Chuwa alikiri uchache wa uzalishaji wa mbegu hizo na kusema kuwa unatokana na uzalishaji wake kuwa mdogo zikiwa shambani kwa mkulima na kufanya wakulima wengi kuvutiwa na kutumia mbegu aina ya TXD 360-Saro 5 ambayo inauwezo wa kuzalisha tani 6-8 kwa hekta.

Amesema, Mbegu ya Saro 5 ambayo ina harufu kidogo kama Aroma ilitokana na mbegu aina ya Supa inayonukia iliyochanganywa na mbegu inayozaa sana kutoka bara la Asia ambayo hainukii na kupata mbegu hiyo aina ya Saro 5 ili kukidhi mahitaji ya mkulima na kuongeza uzalishaji wa mpunga nchini.

Dk. Chuwa amesema kufuatia mbegu aina ya Saro 5 kuonekana kutumika na wakulima walio wengi wataangalia namna ya kuiboresha harufu yake na kuwa na Aroma zaidi na hivyo kufanya walaji kuendelea kupata chakula kizuri na chenye protini kidogo na stachi huku kikiwa na harufu nzuri.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa TARI, Dk. Furaha Mrosso amesema, TARI imeanzishwa nchini ili kuweza kufanya tafiti za msingi zikiwemo za kutumia matokeo ya awali na kupeleka kwa wakulima na Tafiti za kimkakati ambazo wakulima wanapaswa kuzitumia katika kulima kilimo chenye tija.

Dk. Mrosso amesema, teknolojia zilizopo katika vituo sita vya utafiti vilivyopo kanda ya mashariki zina uwezo wa kukidhi malighafi za viwanda vinavyoanza kuendelezwa hapa nchini na hivyo kuwezesha wakulima kunufaika kufuatia mpango wa serikali wa kufanya bei ngazi ya mkulima kuwa juu na kuondokana na umaskini.

Hivyo alitoa rai kwa wakulima kuhakikisha wanapata teknolojia kutoka TARI na kuitumia ili waweze kuongeza uzalishaji na kuondoka katika umaskini.

Naye Ofisa Kiungo utafiti na ugani kanda ya Mashariki TARI, Magreth Mchovu amewashauri wakulima kuhakikisha wanapata elimu ya kutosha ya mazao ya kimkakati ili waweze kujikita katika kilimo hicho kufuatia mazao hayo kuleta manufaa kwenye kilimo.

Aliyataja mazao ya kimkakati kuwa ni pamoja na Michikichi, Pamba, Korosho, Miwa na mbegu za mafuta kama vile Alizeti ambazo alisema zitasaidia kumfanya mkulima kufikia kwenye uchumi wa viwanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!