Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema aliyekamatwa, atoka ‘sero’
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge Chadema aliyekamatwa, atoka ‘sero’

Spread the love

JESHI la Polisi wilayani Tarime limewaachia kwa dhamana, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko (Chadema) na Mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, Sitta Tuma. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).

Matiko na Tuma walikamatwa jana tarehe 8 Agosti, 2018 na Jeshi la Polisi wakiwa kwenye mkutano wa kumnadi mgombea udiwani Chadema Kata ya Turwa.

Polisi waliuzuia mkutano huo kwa sababu ya Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Tarime kuzuia mikutano ya chama hicho.

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Twitter amesema Matiko na Tuma wameachiwa kwa dhamana na kutakiwa kuripoti tena polisi hapo kesho.

Vile vile, Polisi imewaachia kwa dhamana wanachama wa Chadema kumi na nane waliokamatwa jana katika mkutano huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!