Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mahakama Dodoma kutoa hukumu ya kesi ya Kubenea
Habari za Siasa

Mahakama Dodoma kutoa hukumu ya kesi ya Kubenea

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo akiwa nje ya Mahakama ya Dodoma
Spread the love

Mahakama ya wilaya ya Dodoma, imepanga kutoa hukumu ya pingamizi lililowekwa na wakili wa mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea, katika kesi ya jinai inayomkabili katika mahakama hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Pingamizi hilo linahusu nyongeza ya muda wa siku 60 zilizoombwa na serikali, baada ya muda awali kumalizika.

Katika kesi hiyo, Kubenea anadaiwa kumshambulia kwa mateke, ngumi na makofi, Juliana Shonza, mbunge wa Viti Maalum na sasa ambaye amepata uwaziri.

Upande wa mashitaka umeleta maombi hayo kupitia kifungu cha 225 (4) (C) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, Sura ya 20.

Wakili wa utetezi, Isaac Mwaipopo amepinga kuwasilishwa kwa maombi hayo kwa maelezo kuwa yameletwa nje ya muda na kumetumika kifungu kisicho sahihi.

Kwa mujibu wa wakili huyo, kifungu kinachorihusu maombi ya aina hiyo, ni 225 (4) (b).

Amesema maombi ya awali ya nyongeza ya muda yaliwasilishwa mahakamani, tarehe 4 Septemba mwaka jana na hivyo tokea wakati huo, hakuna maombi mengine yoyote yaliyowasilishwa ndani ya muda.

“Mheshimiwa Hakimu, leo ni siku ya 70 tangu serikali kuisha siku 60 za maombi ya serikali. Hivyo basi, maombi haya ya leo, yameletwa mahakamani kinyume na sheria na batili,” ameleza wakili Mwaipopo.

Aliongeza: “Mahakama ni chombo huru na hivyo haipaswi kusumbuliwa na visababu visivyo na msingi. Ninaomba mahakama yako imuachie mshitakiwa na kuifuta kesi hii.”

Baada ya maelezo hayo, Hakimu Mkazi, James Karayemah, amepanga kutoa uamuzi wa pingamizi hilo, tarehe 18 Januari mwaka huu.

Kubenea alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza tarehe 5 Julai mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!