Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA yaihukumu Azam TV, Star TV
Habari Mchanganyiko

TCRA yaihukumu Azam TV, Star TV

Makamu Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Joseph Mapunda
Spread the love

MAMLAKA ya mawasiliono nchini TCRA imetoa hukumu kwa televisheni nne kwa tuhuma za uchochezi  na kukiuka  kanunuzi za utangazaji, Anaripoti Faki Sosi….(endelea)

Mamlaka hiyo kupitia timu yake ya kamati ya maudhui  imevipa adhabu ya kulipa faini  kituo cha televisheni  Star tv, Azam tv Channel ten pamoja na East Africa Tv.

Akisoma hukumu hiyo  hiyo Makamo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Joseph Mapunda amesema kuwa vituo hivyo vimefanya uchochozi kwa kutangaza habari ya kituo cha sheria na  haki za binaadamu kilipokuwa klikitoa tathimini ya uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata 43 uliofanyika  Novemba 30 mwaka 2017 sehemu mbalimbali nchini.

Taarifa ya Kituo cha sheria na haki za binadamu ileelza kuwa  waangalizi wa kituo hicho walifika sehemu mbalimbali zilizofanyika uchaguzi huo na kubaini uvunjwaji wa haki za binadamu, utekwaji na upigwaji wa watu umejitokeza kwenye uchaguzi huo na kwamba vitendo hivyo vimetekelezwa na vyomvo vya dola pamoja na wafuasi wa vyama mbalimbali  vya siasa.

Mapunda ameendelea kusema kuwa vyombo hivyo vilitangaza taarifa hizo bila kuthibitisha ukweli wa taarifa hiyo kwa kuzungumza na wahusika wa wa mamlaka zilizotuhumiwa kama vile Tume ya uchaguzi  NEC au jeshi la Polisi.

Amesema kuwa vyombo hivyo vimepewa adhabu hiyo kutokana kukiuka kanuni za utangazaji , kutangaza habari za uchochezi zingeweza kuhatarisha usalama wa taifa, kutangaza habari ambazo hazikutibitishwa ukweli wake pamoja na  kushindwa kufanya mizania

Hivyo vituo hivyo vimepewa adhabu  ya kulipa faini, vituo hivyo  ni pamoja na  azamu kulipa shilingi 7.5 milioni,  Star tv Shilingi  7.5 milioni na East Afrika tv Shilingi Mil 15milioni pamoja na channel ten 15 milioni.

Mapunda amesema kuwa faini hiyo italipwa ndani ya siku 30 kuanzia leo tarehe 2 januari licha kuwepo wazi kwa rufaa kwa wamiliki wa vyombo hivyo kwa muda wa siku 30 pamoja na kuwekwa chini ya uangalizi kwa muda wa miezi sita kuanzia sasa.

 

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

error: Content is protected !!