Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ndugai uso kwa uso na Lissu, kupelekwa Ulaya J’mosi
Habari za SiasaTangulizi

Ndugai uso kwa uso na Lissu, kupelekwa Ulaya J’mosi

Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki akiwa katika hospitali ya Nairobi kwa matibabu. Picha ndogo Spika wa Bunge Job Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, anatarajiwa kufika mjini Nairobi leo au kesho Alhamisi kumtembelea mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu. Anaripoti Mwandishi Wetu kutoka Nairobi….(endelea).

Taarifa kutoka Bunge la Tanzania na familia ya Lissu jijini Dar es Salaam na mkoani Singida zinathibitisha kuwa Ndugai atakwenda Nairobi kumjulia hali Lissu na kupata taarifa ya matibabu yake.

“Ni kweli kuwa Spika Ndugai atakwenda Nairobi kati ya leo (Jumatano) na kesho Alhamisi kumuona mheshimiwa Lissu. Mipango ya safari hiyo inaratibiwa na familia ya Lissu na baadhi ya marafiki zake wa karibu,” ameeleza mmoja wa wanafamilia wa mbunge huyo.

Amesema, “Ndugai anakwenda Nairobi kuonana na Lissu, kwa lengo la kuzunguza naye juu ya matibabu yake. Anakwenda kwa lengo la kujua maendeleo ya afya ya mbunge huyo na jinsi alivyoathirika na majeraha ya risasi.”

Kupatikana kwa taarifa hizi kumekuja kipindi ambacho, Lissu amekuwa akinukuliliwa kulalamikia Ndugai kuwa “amemtekeleza” Nairobi.

Spika huyo wa Bunge, hajakwenda Nairobi kumuona mbunge wake, tangu mwanasiasa huyo kupelekwa mjini humo Septemba mwaka huu.

Lissu alishambuliwa kwa risasi za moto na wanaoitwa na serikali, “watu wasiofahamika,” nyumbani kwake, majira ya saa saba na nusu mchana akiwa ndani ya gari eneo la Area D, mjini Dodoma.

Kabla ya kupelekwa Nairobi, Lissu alitibiwa katika hospitali ya mkoa wa Dodoma.

Taarifa kutoka familia ya mwanasiasa huyo na Lissu mwenyewe zinasema, mbunge huyo wa Singida Mashariki, anatarajiwa kuondoka mjini Nairobi, Jumamosi wiki hii.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Lissu anapelekwa moja ya nchi za Ulaya, jina na hospitali anayokwenda tunaihifadhi kwa sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!