Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Meya Londa ajisalimisha Urafiki
Habari Mchanganyiko

Meya Londa ajisalimisha Urafiki

Meya wa zamani wa Manispaa ya Kinondoni Alhaji Salum Londa
Spread the love

ALIYEKUWA Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Alhaji Salum Salehe Londa, amelipa deni la pango ya nyumba, analodaiwa na kiwanda cha Nguo cha Urafiki, anaandika Hamisi Mguta.

Taarifa kutoka ndani ya shirika hilo zinasema, Londa alifika makao makuu ya kiwanda hicho yaliyopo maeneo ya Urafiki, barabara ya Morogoro, Ubungo jijini Dar es Salaam, majira ya saa tisa jioni ya leo Jumatano kulipa deni lake.

Londa anadaiwa na kampuni hiyo kiasi cha Sh. 18 milioni ikiwa ni pango la nyumba anayoishi iliyopo eneo la Makaburini, Kinondoni.

Mwandishi wa habari hii, alikutana na Londa ndani ya kiwanda hicho akielekea sehemu ya malipo ili kulipa deni lake.

Habari zinasema Meya Londa amelipa fedha zote Sh. 18 milioni alizokuwa anadaiwa na kiasi gani katika deni analodaiwa na kampuni ya Urafiki.

Awali taarifa zinasema, kampuni hiyo kupitia wakala wake wa kukusanya madeni – Yono Action Mart – ilitoa hadi saa tisa jioni ya leo kwa mwanasiasa huyo wa zamani kulipa deni, vinginevyo angefukuzwa kwenye nyumba hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

error: Content is protected !!