Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Meya Londa ajisalimisha Urafiki
Habari Mchanganyiko

Meya Londa ajisalimisha Urafiki

Meya wa zamani wa Manispaa ya Kinondoni Alhaji Salum Londa
Spread the love

ALIYEKUWA Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Alhaji Salum Salehe Londa, amelipa deni la pango ya nyumba, analodaiwa na kiwanda cha Nguo cha Urafiki, anaandika Hamisi Mguta.

Taarifa kutoka ndani ya shirika hilo zinasema, Londa alifika makao makuu ya kiwanda hicho yaliyopo maeneo ya Urafiki, barabara ya Morogoro, Ubungo jijini Dar es Salaam, majira ya saa tisa jioni ya leo Jumatano kulipa deni lake.

Londa anadaiwa na kampuni hiyo kiasi cha Sh. 18 milioni ikiwa ni pango la nyumba anayoishi iliyopo eneo la Makaburini, Kinondoni.

Mwandishi wa habari hii, alikutana na Londa ndani ya kiwanda hicho akielekea sehemu ya malipo ili kulipa deni lake.

Habari zinasema Meya Londa amelipa fedha zote Sh. 18 milioni alizokuwa anadaiwa na kiasi gani katika deni analodaiwa na kampuni ya Urafiki.

Awali taarifa zinasema, kampuni hiyo kupitia wakala wake wa kukusanya madeni – Yono Action Mart – ilitoa hadi saa tisa jioni ya leo kwa mwanasiasa huyo wa zamani kulipa deni, vinginevyo angefukuzwa kwenye nyumba hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!