Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Vigogo wa almas ‘maji ya shingo’ Kisutu
Habari Mchanganyiko

Vigogo wa almas ‘maji ya shingo’ Kisutu

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

UPELELEZI wa kesi kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Shilingi bilioni mbili inayowakabili vigogo wa madini ya almas umekamilika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, anaandika Faki Sosi.

Watuhumiwa katika kesi hiyo ni mkurugenzi wa tathmini wa madini ya almas, Archard Kalugendo (49) na mtathmini wa madini, Edward Rweyemamu (50) wote wakiwa ni wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini.

Upande wa mashtaka umedai mahakamani hapo kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika kwa sehemu kubwa.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage Wakili wa Serikali Paul Kadushi ameeleza kuwa sehemu kubwa ya upelelezi wa kesi umekamilika, hivyo wanaomba kupangiwa tarehe nyingine.

Hata hivyo, wakili wa utetezi, Nehemiah Nkoko alidai kuwa wamewasilisha maombi ya dhamana katika mahakama ya mafisadi.

Baada ya kueleza hayo, hakimu Mwijage ameahirisha kesi hiyo hadi October 12/2017 mwaka huu.

Kwa pamoja watuhumiwa wakabiliwa na kosa moja la kuisababishia Serikali hasara, wanadaiwa kutenda kosa hilo wamelitenda kati ya August 25 na 31/2017 katika maeneo ya Dar es Salaam na Shinyanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile aukwaa uenyekiti wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

error: Content is protected !!