Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Vigogo wa almas ‘maji ya shingo’ Kisutu
Habari Mchanganyiko

Vigogo wa almas ‘maji ya shingo’ Kisutu

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

UPELELEZI wa kesi kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya Shilingi bilioni mbili inayowakabili vigogo wa madini ya almas umekamilika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, anaandika Faki Sosi.

Watuhumiwa katika kesi hiyo ni mkurugenzi wa tathmini wa madini ya almas, Archard Kalugendo (49) na mtathmini wa madini, Edward Rweyemamu (50) wote wakiwa ni wafanyakazi wa Wizara ya Nishati na Madini.

Upande wa mashtaka umedai mahakamani hapo kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika kwa sehemu kubwa.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage Wakili wa Serikali Paul Kadushi ameeleza kuwa sehemu kubwa ya upelelezi wa kesi umekamilika, hivyo wanaomba kupangiwa tarehe nyingine.

Hata hivyo, wakili wa utetezi, Nehemiah Nkoko alidai kuwa wamewasilisha maombi ya dhamana katika mahakama ya mafisadi.

Baada ya kueleza hayo, hakimu Mwijage ameahirisha kesi hiyo hadi October 12/2017 mwaka huu.

Kwa pamoja watuhumiwa wakabiliwa na kosa moja la kuisababishia Serikali hasara, wanadaiwa kutenda kosa hilo wamelitenda kati ya August 25 na 31/2017 katika maeneo ya Dar es Salaam na Shinyanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!