Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wachimbaji madini wanawake wamlilia Magufuli 
Habari Mchanganyiko

Wachimbaji madini wanawake wamlilia Magufuli 

Spread the love

WACHIMBAJI madini wanawake nchini wameitaka serikali kuwawezesha ili kukuza sekta hiyo inayochangia pato la taifa na kukuza ajira kwa vijana, anaandika Pendo Omary.

Kauli hiyo imetolewa wakati wa warsha ya upatikanaji wa rasilimali zalishi- sekta za ardhi, madini na kilimo zilizofanyika wakati wa tamasha la jinsia la 14 ambalo limeandaliwa na asazi za kiraia, wanaharakati ngazi za jamii na kuratibiwa na TGNP- Mtandao.

Rachel Joseph, Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Madini Wanawake nchini (TAWOMA) ameuambia mtandao wa MwanaHALISI Online  anataka Rais Magufuli awasikie.

Amesema hakuna wanayeshindana naye duniani katika kuchimba madini ya Tanzanite na kwamba wanatakiwa kuchimba kidogokidogo wao  wenyewe.

Amehauri kuwa kwa sasa hakuna  haja ya kuleta wawekezaji kutoka nje, inachopaswa serikali ni kutuwezesha kwa kutupatia ruzuku ili wachimbe kisasa.

Rachel ambaye pia ni kati ya wanawake 30 wanaochimba madini ya Tanzanite Melelani amesema wanawake wachimbaji wanakabiliwa na chanagamoto zaidi kuliko wanaume hivyo wale wanaoweza vizuri kazi hiyo wanapaswa kuwezeshwa ili kuwachochea watoto wa kike kujiajili katika sekta hiyo ili kupunguza tatizo la ajira.

Aidha,   kwa upande wake Sarah Lusambagula, mvumbuzi wa madini ya kombati amesema suala la kupata vibali vya kuendesha shughuli hizo limekuwa ni changamoto.

“Tunapogundua maeneo yenye madini mara baada ya kufanya tafiti, tunalazika kuomba vibali serikalini, lakini tunachokumbana nacho huko ni rushwa na pale unaposhidwa kuwapatia lile eneo uliloligundua anapewa mtu mwingine licha ya kwamba ulikuwa na vigezo vya kupata leseni,” anasema Sara kutoka Wilaya ya Ludewa mkoa wa Njombe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!