HALI ya afya ya Mbunge wa jimbo la Ubungo Saed (Chadema) imebadilika ghafla na kulazimika kupewa mapumziko katika Zahanati ya Bunge kwa ajili ya uangalizi.
Kwa mujibu wa Dk. Noel Salomon, aliyempokea mbunge huyo, Kubenea alifika hopsitalini hapo majira ya saa kumi jioni jana na kupumzishwa .
Dk.Solomon amesema alipatiwa kitanda kwa ajili ya mapumziko ili baadaye apatiwe matibabu.
Jana Kubenea alikuwepo bungeni kuanzia majira ya asubuhi na alikuwa ameishafika katika Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge kwa ajili ya mahojiano kama alivyoagiza Spika wa Bunge, Job Ndugai.
Leave a comment